Friday, February 23, 2018

TAMBUA SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUTOKUFANIKIWA KWA MALENGO YAKO ULIYOJIWEKEA KWA MWAKA 2018



TAMBUA SABABU ZINAZOWEZA   KUPELEKEA  KUTOKUFANIKIWA  KWA  MALENGO YAKO   ULIYOJIWEKEA  KWA  MWAKA  2018

Nipende kumshukuru mwenyezi  Mungu kwa  kutowezesha  kuingia  katika  mwaka  mpya  wa  2018.Pia nikupongeze  wewe  kwa  kuweza  kuwa  miongoni  mwa  waliopewa nafasi  nyingine na Mungu  kuingia mwaka 2018.
Imekuwa kawaida na mazoea  kila mtu kuweka malengo yake mwishoni au mwanzoni  mwa  mwaka kwaajili ya maisha yake na vizazi yake vya baadaye.Hata  hivyo watu wengi  hushindwa kutimiza malengo yao kwa sababu mbalimbali.
Zifuatazo ni sababu  zinazopelekea malengo waliojiwekea watu  walio wengi  kutotimia;

1. KUTOKUANDIKA MALENGO (UNWRITTEN GOALS);
Watu wengi wamekuwa na malengo yaliyowekwa kichwani badala ya kuyaandika sehemu maalum ili iwe rahisi kupitia kila siku na kujua nini wanapaswa kufanya .Kuweka malengo  kichwani ni rahisi kupotea na hutoweza kukumbuka kila  kitu ulichokuwa umekipanga.
Leo  amua kubadilika na kuanza kuandika malengo kwenye notebook yako,kwenye kompyuta yako,kwenye simu yako  na unaweza kwenda mbali zaidi ukayahifadhi mtandaoni hasa kwa njia ya email au vihifadhi vingine kama vile Googledrive ,Dropbox  nakadhalika.

2. KUTOWEKA VIPAUMBILE (LACK OF PRIORITIZATION);
Ukiweka malengo ,ukayaandika  lakini ukashindwa kuweka vipaumbele ni wazi kuwa hutoweza kufikia malengo yako.Vipaumbele hutoa mwelekeo wa nini unapaswa kuanza nacho na kwa nini ,Wakati unapokuwa na lengo zaidi ya moja ni muhimu kukaa chini na kuangalia nini kianze kwa kuangalia umuhimu wake na rasilimali ulizonazo kwa wakati huo.Usipokuwa na vipaumbele utafanya chochote na muda mwingine hata yale ambayo hayako kwenye malengo yako uliyojiwekea.

3.KUTOWEKA UKOMO WA MUDA(NO TIME FRAME/UNBOUNDED GOALS);
Kama umeweka malengo  na malengo  hayo yasiwe na ukomo wa muda ni wazi kwamba huwezi kufikia malengo yako.Utakuwa ni mtu wa kusema nitafanya kesho,Kesho kutwa au hata mwakani kwa sababu hukuweka ukomo wa malengo yako.Ni vema sana ukaanza sasa kuweka muda wa kukamilisha kila lengo nah ii itakusaidia katika kukamilisha malengo yako.

4.KUTOKUWA NA MALENGO HALISIA (UNREALISTIC GOALS);
Kuna watu wanaweka malengo kwa kujifurahisha tu bila kuangalia uhalisia wa malengo hayo kama kweli ni malengo yanayoweza kufikika.Ni muhimu wakati wa kuweka malengo  yako hisia zako ziwe mbali sana.Weka malengo halisi ambayo unaamini yanawezekana baada ya kupima uwezo ulionao.Acha kuweka malengo kwa kunakili au kuiga kwa watu wengine bali weka malengo yako halisia.

5.KUTOKUWA NA MPANGO KAZI KWA  KILA LENGO (LACK OF ACTION PLAN);
Kuweka lengo tu haitoshi,ni muhimu ukaandaa mpango kazi kwa lengo.Kwa mfano umepanga kuanzisha kampuni mwaka huu ni lazima katika lengo hilo utengeneze mpango kazi  utakaoeleza vyanzo  vya pesa vya kuanzisha kampuni hiyo,Watu wanaohitajika katika mchakato ,wahusika wa usajili kama vile wanasheria nakadhalika.Kama hutafanya mambo hayo kwa ufasaha na weledi wa hali ya juu ni vigumu sana kufikia malengo yako ya kuanzisha kampuni.

6.KUTOKUTILIA MANANI(LACK OF COMMITMENT/SERIOUSNESS);
Kama umeweka malengo na hautilii manani hakuna kitakachotokea na mwisho wa siku utakuja na sababu nyingi pamoja na visingizio  vingi vilivyosababisha kutokufikia malengo yako,kumbe wewe ndiwe uliyesababisha malengo yako kutotimia.Ni muhimu sana kama unataka kufika mahali unapotaka kufika ukajenga utamaduni wa kutilia maanani kila ulifanyalo.Hayo ni maisha yako na wewe ndiye nahodha wa maisha yako  mwenyewe na si mwingine kumbuka maisha yako  yapo mikononi mwako mwenyewe.Kama utafanya uvivu ama ulegevu,nakuhakikishia  kuwa  hautatoka kwenye maisha hayo mpaka pale utakapobadilika.

7. KUTOSHIRIKISHA MALENGO(SELFISHNESS/EGOISM);
Watu wengi wanaweka malengo na hawaweki wazi kwa watu wengine huku wakisema malengo ni siri.Iko hivi kama utajiwekea malengo na ushimshirikishe mtu yeyote ni ngumu sana kufikia malengo yako.Unapomshirikisha mtu sahihi malengo yako yeye anaweza kukushauri nini unaweza kufanya na kwa namna ipi ili uweze kufikia malengo yako.Acha kukaa na malengo yako bila kumwambia  mtu yeyote ni  hatari sana na hutakuwa na msukumo wa kuyafikia maana hakuna anayejua.

8.KUTOFANYA TATHMINI(LACK OF EVALUATION);
Kama huna utaratibu wa kukaa chini na kujua nini kimefanyika  mpaka sasa ni ngumu sana kuja kufikia malengo  yako maana hutajua nini kimefanyika na kipi bado hakijafanyika na kifanywe kwa namna ipi.Ni muhimu sasa kama unataka kufika mbali ukaanza kufanya tathmini ya nini umefanya na wapi umeshindwa  na kujua na suluhisho kama kuna changamoto yoyote imejitokeza.

Nakutakia kila la heri katika kukamilisha malengo yako uliyojiwekea katika mwaka huu wa 2018.Usikate tamaa,Usiogope wala usirudi nyuma katika mapambano ya kufikia malengo yako uliyojiwekea(ALUTA CONTINUA)


Makala hii imeandaliwa na kuandikwa  na ;
Samwel  Mohabe Marwa Mbusiro(Mwalimu,Mwinjilisti,Mhubiri ,Mwandishi,Mwanaharakati,Kiongozi ,Mhamasishaji, pamoja  na  Mzungumzaji mbele ya halaiki au mhadhara)-Mwanafunzi chuo kikuu cha afya na sayansi shirikishi Muhimbili(MUHAS)
Simu: 0745325I74/0719200317
Blog:samwelmohabe.blogspot.com
Sanduku la  posta: S.L.P  65001 Dar es salaam,Tanzania
                    23/02/2018.